Wednesday, April 4, 2012

HALIMA MDEE ATANGAZA NIA YAKE YA KUFUNGA NDOA NA NASSARI, Mb. ARUMERU

Halima Mdee Mh. Mbunge wa jamhuri ya muungano wa Tanzania aliejizolea umaarufu mkubwa katika ulimwengu wa siasa nchini, amekua katika macho ya wengi na vyombo vingi vya habari katika shughuri zake na  kwa umaarufu wake katika maisha yake binafsi pia, kwa muda sasa Tumekua tukijiuliza juu ya maisha yake ya kimahusiano au kama dada huyo ana mpenzi? Sasa, Mheshimiwa huyo ameweka wazi juu ya swala hilo na kile nachoweza sema kitawastaajabisha wengi, dada huyo ameweka wazi kua mwenza mteule wake ni Mh. Mbunge mpya wa Arumeru mashariki Mh. Joshua Nassari.

                                                                                                                           
“Nafurahi kwamba Nassari hatimaye ameshinda ubunge katika uchaguzi mdogo,” alisema Mdee wakati akihutubia maelfu ya wakazi wa Arusha na Meru juzi katika viwanja vya Leganga kusherehekea ushindi wa chama chake katika uchaguzi huo.

Mdee alifafanua, kwamba yeye na chama chake walikuwa wamebanwa na kampeni za kuhakikisha Chadema inatwaa jimbo la Arumeru Mashariki na ndiyo sababu hakujibu mara moja maombi ya Nassari ya kumwoa aliyoyatoa katika moja ya mikutano yake ya kampeni.

“Naondoka kwenda Dar es Salaam kujiandaa kwa Mkutano ujao wa Bunge, kisha nitakwenda Dodoma ambako nitamsubiri Nassari na kwa pamoja tutafanya maandalizi,” alisema Mdee huku akishangiliwa na hadhira hiyo huku wakiimba na kucheza katikati ya mvua iliyokuwa ikinyesha.

Mdee alisema ndoa kati ya wabunge hao wawili wa Chadema ni wazo zuri na itatangazwa sana na kuandika historia.

Alipoona anashambuliwa sana na wapinzani wake juu ya useja wake katika kampeni hizo, Nassari hatimaye alitangaza kumwoa Mdee ambaye pia hajaolewa

No comments:

Post a Comment

Infolinks In Text Ads

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

we gOt friends too